UTUME WA KANISA

TAMKO LA UTUME LA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO

Utume Wetu

 Kuwafanya watu wote kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo, wanaoishi kama mashahidi Wake wa upendo na kutangaza kwa watu wote injili ya milele ya Ujumbe wa Malaika Watatu, kwa ajili ya maandalizi ya kurudi Kwake hivi karibuni (Mathayo 28:18-20, Matendo 1:8, Ufunuo 14:6-12).

Njia Yetu ya Utekelezaji

Tukiongozwa na Biblia na Roho Mtakatifu, Waadventista wa Sabato hutekeleza utume wa kuwafanya watu kuwa wanafunzi kupitia maisha ya mfano wa Kristo, uponyaji, huduma, kutangaza, kufundisha, na kutoa mafunzo ya vitendo.

Maono/Njozi Yetu

Kwa kupatana na ufunuo wa Biblia, Waadventista wa Sabato huona kilele cha mpango wa Mungu wa urejeshwaji wa viumbe vyake vyote katika umoja kamili na mapenzi yake makamilifu na haki Yake.